Friday, September 19, 2014

KUKAA KWA AMANI NA MWAJIRI

Mungu hupenda watu wa aminifu kwa  wa ajiri wao. Kama ume ajiriwa unapaswa kuzingatia yafuatayo:

1. Ukiwa kazini tumia muda vizuri. Siyo vizuri kutumia muda mwingi kwa simu,maongezi na marafiki au kwa matembezitembezi ndani ya masaa ya kazi. Hakikisha unafanya kazi kwa manufaa ya mwajiri/kampuni katika masaa yako ya kazi kwa mujibu wa mkataba wako wa kazi.

2.Siyo tabia nzuri kutumia mali ya mwajiri vibaya kama vile, umeme N.K kwa matumizi binafsi, marafiki au jamaa zako. Dhamini mali ya mwajiri kama unavyo dhamini mali yako mwenyewe kwani huwezi kufurahia kutapanya mali yako ovyo ovyo.Kumbuka mwajiri anatoa gharama kununua hizo mali kwa manufaa ya kampuni kama unavyo gharimia mali za nyumbani kwako kwa manufaa ya familia yako.

3. Usifanye mahali pa kazi ni mahali pa kukutania na marafiki kwa maongezi yenu binafsi.

4. Ukiwa kiongozi usitumie madaraka yako uliyopewa kuwagandamiza au kuwanyanyasa wengine hata kuwalazimisha kufanya maovu, kama vile mapenzi au kuwatumia kufanya mambo yako binafsi kwa uonevu.

Tumwombe Mungu atuwezeshe kuwa wa aminifu kwa kila jambo.

Tuesday, September 9, 2014

KUTOKA MAUTI HADI UZIMA WA MILELE

YESU KRISTO alikuja ili kila amwaminiye asipotee ila awe na uzima wa milele.

 Jambo lililomleta Mwana wa Mungu duniani ni Kumkomboa mwanadamu aliyetenda dhambi kutoka katika dhambi zake na kufanywa mwana wa Mungu na kuwa mtakatifu kama baba wa mbinguni alivyo.

Roho mtakatifu anamwezesha aliye amini kuishinda dhambi.  Tumruhusu roho wa kweli atuongoze kwa kwenda kwa roho ili tusizitimize tamaa za mwili kwani mwili hutamani kushindana na roho ila tuki ufuata mwili tutabaki mautini hivyo imempasa kila anayeitwa kwa jina la Kristo kuenenda kama yeye alivyo enenda alipokuwa hapa duniani na kutuachia kielelezo.

Endelea kutembelea hapa tujifunze mapenzi ya Baba wa Mbinguni ili tuweze kuyafanya kwani watakao karibishwa mbinguni siku ya mwisho si wale wanaosema Bwana Bwana ila wanao yafanya mapenzi ya Mungu.

YESU KRISTO NI LANGO PEKEE LA KUINGILIA MBINGUNI

MSIPO INYWA DAMU YANGU NA KUULA MWILI WANGU HAMTAWEZA KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU.
Maneno hayo ni roho na walio wa rohoni watayatekeleza kiroho.

*Maana ya kunywa Damu ya Yesu Kristo kiroho:
Ndani ya Damu ndimo mlimo UHAI. Sote tumefanya dhambi na kustahili mauti kwani mshahara wa Dhambi ni mauti, ila Karama ya MUNGU ni UZIMA WA MILELE ULIO KATIKA KRISTO YESU.Tunapo mkiri Yesu Kuwa MWOKOZI WA MAISHA YETU KWA KUTUBU DHAMBI ZETU NA KUREJEA KWA KUJISALIMISHA NIA ZETU KWA NIA YA KRISTO INAYOTII DAIMA MAPENZI YA MUNGU KATIKA HALI ZOTE; Tunakubali kafara yake Msalabani kama fidia ya dhambi zetu na hapo hapo  kifo cha Yesu msalabani huwa badala ya dhambi zetu na Sisi kuhesabiwa haki ya KRISTO KANA KWAMBA HATUJAWAHI KUTENDA DHAMBI HIVYO KUSTAHILI UZIMA WA MILELE.
TUNACHUKUA ROHO YA KRISTO. Ee MUNGU UTUPE ROHO YA KRISTO KWA WINGI MAISHANI MWETU.

*Maana ya kula mwili wa kristo kiroho:
Kristo ni NENO hivyo tukijazwa na Neno la Mungu nafsini mwetu na kuli ishi, Tuna ushiriki mwili mtukufu wa Kristo unaoweza kushinda MAJARIBU na Dhambi. Yesu ali ishi kwa kupitia Majaribu kama sisi lakini hakutenda dhambi hivyo kwa neema yake kama tutajikana nafsi na kumfuata tutaishinda dhambi na kuishi maisha matakatifu kama YEYE Alivyo ishi alipokuwa hapa Duniani. Tunapo mkiri Yesu Kuwa BWANA WA MAISHA YETU KWA KUISHI KWA KILA NENO LITOKALO KINYWANI MWA BWANA Ndipo Maisha ya Yesu yanakuwa kielelezo kwetu wakristo.UKIITWA  MKRISTO SHARTI UISHI MAISHA MATAKATIFU KAMA KRISTO. Ee MUNGU TUWEZESHE KUJAZWA NENO LAKO NA KULI ISHI ILI TUKAE KATIKA PENDO LAKO KAMA KRISTO BWANA WETU. AMINA.

YATUPASA KUZIACHA NJIA ZETU NA KUFUATA KILA NJIA INAYOELEKEZWA NA NENO LA MUNGU ILI TUPATE KUISHI.