Tuesday, September 9, 2014

KUTOKA MAUTI HADI UZIMA WA MILELE

YESU KRISTO alikuja ili kila amwaminiye asipotee ila awe na uzima wa milele.

 Jambo lililomleta Mwana wa Mungu duniani ni Kumkomboa mwanadamu aliyetenda dhambi kutoka katika dhambi zake na kufanywa mwana wa Mungu na kuwa mtakatifu kama baba wa mbinguni alivyo.

Roho mtakatifu anamwezesha aliye amini kuishinda dhambi.  Tumruhusu roho wa kweli atuongoze kwa kwenda kwa roho ili tusizitimize tamaa za mwili kwani mwili hutamani kushindana na roho ila tuki ufuata mwili tutabaki mautini hivyo imempasa kila anayeitwa kwa jina la Kristo kuenenda kama yeye alivyo enenda alipokuwa hapa duniani na kutuachia kielelezo.

Endelea kutembelea hapa tujifunze mapenzi ya Baba wa Mbinguni ili tuweze kuyafanya kwani watakao karibishwa mbinguni siku ya mwisho si wale wanaosema Bwana Bwana ila wanao yafanya mapenzi ya Mungu.

No comments:

Post a Comment