Tuesday, September 9, 2014

YESU KRISTO NI LANGO PEKEE LA KUINGILIA MBINGUNI

MSIPO INYWA DAMU YANGU NA KUULA MWILI WANGU HAMTAWEZA KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU.
Maneno hayo ni roho na walio wa rohoni watayatekeleza kiroho.

*Maana ya kunywa Damu ya Yesu Kristo kiroho:
Ndani ya Damu ndimo mlimo UHAI. Sote tumefanya dhambi na kustahili mauti kwani mshahara wa Dhambi ni mauti, ila Karama ya MUNGU ni UZIMA WA MILELE ULIO KATIKA KRISTO YESU.Tunapo mkiri Yesu Kuwa MWOKOZI WA MAISHA YETU KWA KUTUBU DHAMBI ZETU NA KUREJEA KWA KUJISALIMISHA NIA ZETU KWA NIA YA KRISTO INAYOTII DAIMA MAPENZI YA MUNGU KATIKA HALI ZOTE; Tunakubali kafara yake Msalabani kama fidia ya dhambi zetu na hapo hapo  kifo cha Yesu msalabani huwa badala ya dhambi zetu na Sisi kuhesabiwa haki ya KRISTO KANA KWAMBA HATUJAWAHI KUTENDA DHAMBI HIVYO KUSTAHILI UZIMA WA MILELE.
TUNACHUKUA ROHO YA KRISTO. Ee MUNGU UTUPE ROHO YA KRISTO KWA WINGI MAISHANI MWETU.

*Maana ya kula mwili wa kristo kiroho:
Kristo ni NENO hivyo tukijazwa na Neno la Mungu nafsini mwetu na kuli ishi, Tuna ushiriki mwili mtukufu wa Kristo unaoweza kushinda MAJARIBU na Dhambi. Yesu ali ishi kwa kupitia Majaribu kama sisi lakini hakutenda dhambi hivyo kwa neema yake kama tutajikana nafsi na kumfuata tutaishinda dhambi na kuishi maisha matakatifu kama YEYE Alivyo ishi alipokuwa hapa Duniani. Tunapo mkiri Yesu Kuwa BWANA WA MAISHA YETU KWA KUISHI KWA KILA NENO LITOKALO KINYWANI MWA BWANA Ndipo Maisha ya Yesu yanakuwa kielelezo kwetu wakristo.UKIITWA  MKRISTO SHARTI UISHI MAISHA MATAKATIFU KAMA KRISTO. Ee MUNGU TUWEZESHE KUJAZWA NENO LAKO NA KULI ISHI ILI TUKAE KATIKA PENDO LAKO KAMA KRISTO BWANA WETU. AMINA.

YATUPASA KUZIACHA NJIA ZETU NA KUFUATA KILA NJIA INAYOELEKEZWA NA NENO LA MUNGU ILI TUPATE KUISHI.


 

No comments:

Post a Comment