Wokovu ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
Upendo wa Kweli hujulikana kwa matendo yake. wakati mwingine kama binadamu tunaweza kusema tunampenda mtu fulani , wakati matendo yetu yanadhihirisha kinyume chake.(Yohana 3:17,18). Hilo kwa Mungu haliwezi kutokea. Upendo wake unaakisiwa katika matendo yake. kutokana na upendo, alimtoa Mwana wake wa pekee kwa ajili ya wokovu wetu. Kwa kufanya hivyo, Mungu alitupatia vyote alivyo navyo, ambavyo ni Yeye mwenyewe.
Upendo wa Mungu haubagui, au hata kutegemea matendo yetu. Mungu anaupenda ulimwengu, huku ni kusema, binadamu wote, pamoja na wale wasiompenda.
Soma Luka 18:9-14. Huenda tumeusoma mfano huu lakini hatushangazwi na hukumu ya Yesu:"Nawa ambia, huyu (mtoza ushuru) alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule" (luka 18:14) . Hata hivyo , wale waliomsikia Yesu akitamka hukumu hii lazima walishangazwa. Je, haya hayakuwa matokeo yasiyo ya haki? Ndiyo, hakustahili kabisa. Hivi ndivyo wokovu ulivyo. Ni zawadi kutoka kwa Mungu.Zawadi hazifanyiwi kazi ila tu huwa zinapokelewa/zinakubaliwa. Hatuwezi kununua wokovu; tunaweza tu kuupokea. Ingawa Yesu alitumia neno Neema kwa nadra, lakini alifundisha waziwazi kwamba wokovu ni kwa njia ya Neema, na Neema ni kupewa kile usichostahili.
Tumwombe Mungu atuwezeshe kuipokea zawadi ya wokovu kama Mtoza Ushuru na Tusi ikatae kwa kudhani ni haki yetu kama mfarisayo alivyofanya. Sote tumetenda dhambi na kuhitaji zawadi ya wokovu. Hakuna hata mmoja anayeweza kujiokoa mwenyewe tangu Adamu alipo tenda dhambi kwani sote tulitumbukia shimoni na kumhitaji Mwokozi ambaye hajawahi kutenda dhambi yaani Kristo peke yake.
akiisha kutukomboa kutoka katika shimo la dhambi Kristo anatualika kuishi maisha ya utakatifu kama Yeye mwenyewe alivyoishi kwa kuzishika Amri za Mungu hivyo kuyafanya mapenzi ya Baba yake siku zote na Kukaa katika Pendo la Baba wa Mbinguni.
usikose sehemu ya tatu ya somo hili ujifunze maarifa kamili ya wokovu.
Friday, October 10, 2014
Wednesday, October 8, 2014
JINSI YA KUOKOLEWA-Sehemu ya kwanza
"Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele" (Yohana 3:16)
"Kifo" huwa tunasema, 'ni sehemu tu ya maisha." Hapana, Kifo ni kinyume cha maisha, siyo sehemu yake. Lakini kwa kuwa tumekizoea sana kifo tunaona hivyo kinyume na uhalisi wake. vyovyote tutakavyo elewa ,
jambo moja ni la hakika: Bila msaada wa Mungu, Kifo cha milele kingekuwa ndio mwisho wetu wote.
Kwa bahati nzuri, msaada huo umekuja. Mungu katika upendo wake usio na ukomo, anatupatia wokovu kwa njia ya Kristo. wakati malaika alipotangaza kuzaliwa kwa masihi, alimwita YESU ambalo ni neno la kiebrania lenye maana ya Wokovu. maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao (Mathayo 1:21)
katika somo hili la jinsi ya kuokolewa tutatafakari kazi ya Yesu ya kuokoa. Tutajielekeza katika msingi wa wokovu wetu na baadaye katika matokeo yake.
Biblia iko wazi. Tuna uchaguzi wa aina mbili tu kuhusu dhambi zetu,
1. Tunakubali malipo ya Kristo kwa ajili ya dhambi zetu katika msalaba wa Kalvari, AU
2. Tunazilipia dhambi zetu kwenye ziwa la moto katika mauti ya pili
Kwa wanaokubali kumwamini Kristo kwa kushika Amri za Mungu na Imani ya kristo (ufunuo 12:17) mauti ya pili haina nguvu. Kadiri tunavyopitia tena zawadi ya neema ya Mungu kwa njia ya Kristo, hebu kwa unyenyekevu tuifanye upya tena Imani yetu kwa Yesu kama Mwokozi wetu binafsi.
Endelea kutembelea katika sehemu ya pili ya somo hili upate ufunguo wa maarifa ya maisha ya wokovu.
UBARIKIWE NA BWANA.
"Kifo" huwa tunasema, 'ni sehemu tu ya maisha." Hapana, Kifo ni kinyume cha maisha, siyo sehemu yake. Lakini kwa kuwa tumekizoea sana kifo tunaona hivyo kinyume na uhalisi wake. vyovyote tutakavyo elewa ,
jambo moja ni la hakika: Bila msaada wa Mungu, Kifo cha milele kingekuwa ndio mwisho wetu wote.
Kwa bahati nzuri, msaada huo umekuja. Mungu katika upendo wake usio na ukomo, anatupatia wokovu kwa njia ya Kristo. wakati malaika alipotangaza kuzaliwa kwa masihi, alimwita YESU ambalo ni neno la kiebrania lenye maana ya Wokovu. maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao (Mathayo 1:21)
katika somo hili la jinsi ya kuokolewa tutatafakari kazi ya Yesu ya kuokoa. Tutajielekeza katika msingi wa wokovu wetu na baadaye katika matokeo yake.
Biblia iko wazi. Tuna uchaguzi wa aina mbili tu kuhusu dhambi zetu,
1. Tunakubali malipo ya Kristo kwa ajili ya dhambi zetu katika msalaba wa Kalvari, AU
2. Tunazilipia dhambi zetu kwenye ziwa la moto katika mauti ya pili
Kwa wanaokubali kumwamini Kristo kwa kushika Amri za Mungu na Imani ya kristo (ufunuo 12:17) mauti ya pili haina nguvu. Kadiri tunavyopitia tena zawadi ya neema ya Mungu kwa njia ya Kristo, hebu kwa unyenyekevu tuifanye upya tena Imani yetu kwa Yesu kama Mwokozi wetu binafsi.
Endelea kutembelea katika sehemu ya pili ya somo hili upate ufunguo wa maarifa ya maisha ya wokovu.
UBARIKIWE NA BWANA.
Subscribe to:
Posts (Atom)