Wokovu ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
Upendo wa Kweli hujulikana kwa matendo yake. wakati mwingine kama binadamu tunaweza kusema tunampenda mtu fulani , wakati matendo yetu yanadhihirisha kinyume chake.(Yohana 3:17,18). Hilo kwa Mungu haliwezi kutokea. Upendo wake unaakisiwa katika matendo yake. kutokana na upendo, alimtoa Mwana wake wa pekee kwa ajili ya wokovu wetu. Kwa kufanya hivyo, Mungu alitupatia vyote alivyo navyo, ambavyo ni Yeye mwenyewe.
Upendo wa Mungu haubagui, au hata kutegemea matendo yetu. Mungu anaupenda ulimwengu, huku ni kusema, binadamu wote, pamoja na wale wasiompenda.
Soma Luka 18:9-14. Huenda tumeusoma mfano huu lakini hatushangazwi na hukumu ya Yesu:"Nawa ambia, huyu (mtoza ushuru) alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule" (luka 18:14) . Hata hivyo , wale waliomsikia Yesu akitamka hukumu hii lazima walishangazwa. Je, haya hayakuwa matokeo yasiyo ya haki? Ndiyo, hakustahili kabisa. Hivi ndivyo wokovu ulivyo. Ni zawadi kutoka kwa Mungu.Zawadi hazifanyiwi kazi ila tu huwa zinapokelewa/zinakubaliwa. Hatuwezi kununua wokovu; tunaweza tu kuupokea. Ingawa Yesu alitumia neno Neema kwa nadra, lakini alifundisha waziwazi kwamba wokovu ni kwa njia ya Neema, na Neema ni kupewa kile usichostahili.
Tumwombe Mungu atuwezeshe kuipokea zawadi ya wokovu kama Mtoza Ushuru na Tusi ikatae kwa kudhani ni haki yetu kama mfarisayo alivyofanya. Sote tumetenda dhambi na kuhitaji zawadi ya wokovu. Hakuna hata mmoja anayeweza kujiokoa mwenyewe tangu Adamu alipo tenda dhambi kwani sote tulitumbukia shimoni na kumhitaji Mwokozi ambaye hajawahi kutenda dhambi yaani Kristo peke yake.
akiisha kutukomboa kutoka katika shimo la dhambi Kristo anatualika kuishi maisha ya utakatifu kama Yeye mwenyewe alivyoishi kwa kuzishika Amri za Mungu hivyo kuyafanya mapenzi ya Baba yake siku zote na Kukaa katika Pendo la Baba wa Mbinguni.
usikose sehemu ya tatu ya somo hili ujifunze maarifa kamili ya wokovu.
No comments:
Post a Comment