"Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele" (Yohana 3:16)
"Kifo" huwa tunasema, 'ni sehemu tu ya maisha." Hapana, Kifo ni kinyume cha maisha, siyo sehemu yake. Lakini kwa kuwa tumekizoea sana kifo tunaona hivyo kinyume na uhalisi wake. vyovyote tutakavyo elewa ,
jambo moja ni la hakika: Bila msaada wa Mungu, Kifo cha milele kingekuwa ndio mwisho wetu wote.
Kwa bahati nzuri, msaada huo umekuja. Mungu katika upendo wake usio na ukomo, anatupatia wokovu kwa njia ya Kristo. wakati malaika alipotangaza kuzaliwa kwa masihi, alimwita YESU ambalo ni neno la kiebrania lenye maana ya Wokovu. maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao (Mathayo 1:21)
katika somo hili la jinsi ya kuokolewa tutatafakari kazi ya Yesu ya kuokoa. Tutajielekeza katika msingi wa wokovu wetu na baadaye katika matokeo yake.
Biblia iko wazi. Tuna uchaguzi wa aina mbili tu kuhusu dhambi zetu,
1. Tunakubali malipo ya Kristo kwa ajili ya dhambi zetu katika msalaba wa Kalvari, AU
2. Tunazilipia dhambi zetu kwenye ziwa la moto katika mauti ya pili
Kwa wanaokubali kumwamini Kristo kwa kushika Amri za Mungu na Imani ya kristo (ufunuo 12:17) mauti ya pili haina nguvu. Kadiri tunavyopitia tena zawadi ya neema ya Mungu kwa njia ya Kristo, hebu kwa unyenyekevu tuifanye upya tena Imani yetu kwa Yesu kama Mwokozi wetu binafsi.
Endelea kutembelea katika sehemu ya pili ya somo hili upate ufunguo wa maarifa ya maisha ya wokovu.
UBARIKIWE NA BWANA.
No comments:
Post a Comment