KUTAMBUA KUNDI LA MUNGU DUNIANI
Mamlaka za kiserikali hutuambia ya kwamba ni rahisi sana kutofautisha kati ya noti ya fedha ya
kweli na ile ya bandia. Unaona, wao hujifunza tabia ya ile note ya kweli kwa undani.Wanajua wembamba na mpangilio wa vijinyuzi vidogo sana vitengenzavyo karatasi, wepesi au uzito wa rangi au wino, nembo na utaratibu halali wa nambari za fedha iliyo halisi na ya kweli. (elezea fedha)! Wanapoitizama noti,
wanalinganisha upesi na zile sifa zitambulishazo fedha iliyo halali. Kama inapungukiwa sifa yoyote katika zile zilizo katika iliyo halali, basi inakuwa bandia.
Vivyo hivyo na kweli.
Hatuhitaji kujifunza mafundisho ya madhehebu yote kwa muda mrefu, kama tunajua tabia za kanisa la kweli la Mungu kama zilivyotajwa katika Biblia.!
Mungu hamuachi mwanadamu akisie kuwa ni ipi dini ya kufuata, kwani Mungu ametupatia kweli katika Neno lake: Hakika Bwana MUNGU !hatafanya neno lolote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.!Amosi 3:7
Kitabu cha Ufunuo ni muhtasari wa unabii wote katika Biblia. Kinawapatia watu mtizamo wa pekee wa siku ya mwisho.!Hapa mchafuko wa uasi na dini uliopo katika siku za mwisho za historia ya Dunia unafunuliwa.!
Ufunuo unatabiri juu ya pambano kati ya kanisa la Kristo na Shetani.!Sura ya 12 inatoa picha kama filamu ya historia ya kanisa tangu wakati wa Kristo hadi mwisho wa dunia:
NEEMA YA BWANA WETU YESU KRISTO IWE PAMOJA NAWE, NA BWANA ATUFUNULIE KWELI YOTE KWA MSAADA WA ROHO MTAKATIFU.AMINA.
No comments:
Post a Comment