KUWAITA VIJANA WOTE!
Maana ndiwe taraja langu, Ee Bwana MUNGU, Tumaini langu tokea ujana wangu. Zaburi 71:5.
Yesu anamwita kila mpotevu, akisema, "Mwanangu, nipe moyo wako." Mithali 23:26....
Vijana hawawezi kuwa na furaha bila kuwa na upendo wa Yesu. Anangoja kwa huruma
kusikiliza maungamo ya wale walio watundu, na kuikubali toba yao. Anatazamia
kurudishiwa shukrani toka kwetu, kama vile mama anavyotazamia kuona tabasamu ya
kumtambua toka kwa mtoto wake ampendaye sana. Mungu aliye mkuu anatufundisha sisi
kumwita yeye Baba. Angependa sisi tuelewe jinsi moyo wake kwa dhati na kwa upole
unavyotupenda sana tunapokuwa katika maonjo na majaribu yetu....
Vijana wangekuwa wanaendelea daima kukua katika neema, na katika ujuzi wa ile
kweli. Muumbaji wa vitu vyote, ambaye hazina zote za hekima anazo, ameahidi kuwa
kiongozi wetu katika ujana wetu. Yeye aliyezishinda nguvu zote za uovu kwa ajili yetu
anatutaka tumsujudie. Hapawezi kuwapo na ujuzi wa juu kuliko ule wa kumjua Yeye
ambaye kumjua vema ni uzima na amani; hakuna upendo ulio safi na wenye kina kuliko
upendo ule wa Mwokozi wetu.
Kuna majaribu kila upande kuinasa miguu ya wale wasiojihadhari. Vijana wale
wasiomcha Mungu, wenye matendo mabaya wanao mvuto wenye nguvu kuwaongoza
wengine katika njia zile zilizokatazwa. Hao ni miongoni mwa vibaraka wa Shetani
wanaofanikiwa sana.... Mara nyingi wapenda dunia hii watakuja katika vazi la kirafiki, na
kujaribu kuingiza desturi na matendo yake. Hebu kila askari wa kweli awe tayari
kuvipinga vishawishi hivyo.
Shetani hutushambulia mahali pale tulipo na udhaifu; lakini hatuna haja ya kushindwa.
Shambulio hilo laweza kuwa kali na la muda mrefu, lakini Mungu ameahidi kutupatia
msaada wake, na kwa nguvu zake sisi tunaweza kushinda.... Kanuni na ahadi za neno la
Mungu zitatupatia silaha zenye uwezo wa Mungu kumpinga adui huyo.... Shetani
atachanganyikiwa na kushindwa anapokuta moyo wako
unajishughulisha na kweli ya Mungu. Pia mara kwa mara tunahitaji kuonekana kwenye
kiti kile cha neema. Maombi ya bidii na ya kudumu, yakiunganisha udhaifu wetu wa
kibinadamu na Uweza usio na kikomo wa Mungu, yatatupatia ushindi.
SOMA HABARI ZINAZOCHAPISHWA KATIKA BLOG HII UPATE NURU KUTOKA MBINGUNI
No comments:
Post a Comment