Wednesday, May 28, 2014

UNAWEZAJE KUMKANA KRISTO?

  • Tunaweza kumkana kwa maneno yetu na kwa kusema mabaya juu ya wengine kwa mazungumzo ya upuzi, ubishi na maneno ya mzaha.
  • Kwa maneno ya bure, yasiyo na maana au maneno makali ama kwa kusema uongo, kinyume cha kweli. kwa maneno yetu tunaweza kuonyesha kuwa kristo hayupo ndani yetu.
  • Kwa tabia yetu tunaweza kumkana Kristo kwa kupenda raha ,kwa kuepuka kazi na mizigo ya maisha ambayo mtu mwingine hana budi kuichukua kama sisi tusipoichukua.
  •  Kwa kiburi cha nguo tuvaazo ,kwa kufuata mtindo wa ulimwengu au kwa mwenendo mbaya usio na adabu. 1Petro3:3-5.
  • Kwa kupendelea maoni yetu wenyewe na kujaribu kuudumisha utu wa kale au kujihesabu wenyewe kuwa wenye haki.

Usalama tu kwa vijana ni kukesha kila wakati na kuomba kwa moyo mnyenyekevu. Kama twafanya hivyo malaika hutazama sala zetu, na ikiwa sala hizo hazijatoka katika midomo ya kusingizia wakati tukiwa katika hatari ya kufanya mabaya bila kujua na kutoa mvuto utakaowaongoza wengine kufanya mabaya, malaika atulindae atakuwa karibu nawe  kukusaidia kutenda mema, akikuchagulia maneno, na kuongoza matendo yako.Zaburi 5:3-4 .
soma Mithal 3:3-4, 2Timotheo 2:19, Waebrania 12:14.

No comments:

Post a Comment