UJUMBE MAALUM KWA VIJANA.
UZITO WA NENO "NAKUPENDA"
Katika mawazo na fikra nyingi za vijana wa kileo neno, "NAKUPENDA" linatumika vibaya sana bila kuzingatia muda, mahali na hata kiwango au hadhi ya mtu unayemuambia kuwa unampenda.
Neno hilo limekuwa kama salamu tu, bila shaka ni kama mtu anaposema shikamoo! limekuwa ni kigezo kikubwa cha kuwalaghai wasichana kisha kuwachezea na baadaye kuwaacha. Wasichana wengi nao wanapotamkiwa neno "NAKUPENDA" wanachanganyikiwa kabisa, linawavuruga kabisa mfumo wa fahamu na kuwanyima uwezo wa kufikiri tena juu ya maisha yao ya baadaye kwani wanajiona wao ndio wao, kitakachofuata baada ya hapo ni "NAKUPENDA PIA" na baadaye neno "NDIYO" katika kila jambo.
Sasa basi, kwa nini wewe kijana wa kiume uliyelelewa na kufunzwa adabu njema, umtamkie msichana kuwa UNAMPENDA wakati huna uhakika na hisia zako na humaanishi unachokisema? Kwa nini basi usitumie neno "NAKUPENDA" wakati wa ndoa yako utakapowadia? Au kwa nini neno hili lisitumike katika kujenga mahusiano ya kawaida tu?
Tafakari kwa makini, unatakiwa kuwa na uhakika wa hisia zako.
Kwa akina dada nao, kwa nini ukubali kudanganyika eti kwa vile mtu amekuambia anakupenda? Tuwe makini kutamka neno hili na tutafakari jinsi ya kulipokea.
TEMBELEA BLOG HII KILA SIKU UPATE HEKIMA KUTOKA JUU MBINGUNI.
No comments:
Post a Comment