SWALI:
NI NANI ALIYEFUNULIWA KATIKA MAANDIKO MATAKATIFU YOTE?
JIBU:
YESU KRISTO,
"Mwayachunguza maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake;na hayo ndiyo yanayonishuhudia" Yoh.5:39.
Biblia nzima ni ufunuo wa kazi ya Kristo, hasa wa kazi yake ulimwenguni kwa ajili ya wanadamu. Kristo aliwafundisha wanafunzi wake juu yake mwenyewe kwa Maandiko ya Agano la Kale."Akaanza kutoka Musa na manabii wote,akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe" Luka 24:27.
FAHAMU KWAMBA:
YESU KRISTO WA NAZARETH NDIYE NJIA,KWELI NA UZIMA.YEYOTE AJAE KWAKE ATAPATA MAJI YA UZIMA BURE.
IJUE KWELI NAYO KWELI ITAKUWEKA HURU! BIBLIA YOTE KUANZIA KITABU CHA MWANZO HADI KITABU CHA UFUNUO NI NENO LA KRISTO NA NENO LAKE NDIYO KWELI.
SWALI:
Mwalimu mwema nifanye nini ili ni uridhi UFALME WA MUNGU?
JIBU:
Yesu akajibu, Je,wazijua AMRI?Soma Kutoka 20:1-17(AMRI KUMI ZA MUNGU). Kijana akajibu Hizo nimezishika toka utoto wangu.
Yesu akampenda akamwambia Kauze mali zako uwape maskini kisha unifuate.
FAHAMU KWAMBA:
INATUPASA KUZISHIKA AMRI ZA MUNGU NA KUMFUATA KRISTO ILI TUWEZE KU URIDHI UFALME WA MUNGU (ku upata uzima wa milele)
TAFUTENI KWANZA UFALME WA MUNGU NA HAKI YAKE NA MENGINE MTAZIDISHIWA.
TEMBELEA BLOG HII KILA SIKU UJIFUNZE MAMBO MUHIMU ILI UWEZE KUPATA UZIMA WA MILELE
"Basi, enendeni,kawafanyeni mataifa yote kuwa wanafunzi,.. mkiwafundisha kushika yote niliyowaamuru ninyi: na tazama,mimi nipo pamoja nanyi siku zote,hata mwisho wa dunia" Alisema Bwana wetu.
Ameen
ReplyDeleteAmen
ReplyDeleteAmen
ReplyDelete